STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 22, 2013

Mbunge wa Kigamboni katika Jogging

Jua lile literemke mamaaa aiyaa iyaaa iaayyaa mmaaaaamaaa! Ni kama Mbunge wa KIgamboni Faustine Ndugulile akiwaongoza baadhi ya wapiga kura wake na wanamichezo wengine katika Jogging iliyofanika leo Mbagala
Na Moshi Lusonzo
MBUNGE wa jimbo la Kigamboni, jijini Dar es Salaam, Dk. Faustine Ndugulile,amewataka vijana kujikita kwenye michezo michezo mbalimbali kama sehemu ya ajira pamoja na kujenga afya zao.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya mwaka mmoja wa Klabu ya mchezo wa mbio za pole (Jogging) ya Mbagala, Dk. Ndgulile, alisema endapo vijana hao watabadilika kimtazamo, yeye binafsi atajitolea kuwasaidia ili kuinuka kiuchumi.

Alisema wakati vijana kugeuza vikundi hivyo kuwa sehemu ya kufanyia uhuni na vitendo viovu umekwisha, badala yake watumie nafasi hiyo kujielemisha na kuibua mawazo yatayopelekea miradi ya kimaendeleo.

"Nawapongeza wanachama wa Mbagala Jogging kwa kufikisha muda wa mwaka mmoja mpo pamoja, lakini nawasihi kwa muda huu muanze kufikiria ndani ya kikundi mtafanya nini kwa ajili ya maendeleo yenu," Alisema

Dk. Ndugulile, aliahidi kusaidia kikundi hicho jezi kwa ajili ya mazoezi  pamoja na mtaji wa mradi wowote watakaopendekeza.

Akisoma risala, Kiongozi wa kikundi hicho, Time Saidi, alisema Kikundi hicho chenye vijana 116 kimefanikiwa kuwaweka pamoja vijana na kuwaepusha na tabia ya matumizi ya madawa ya kulevya.

 

No comments:

Post a Comment