STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 22, 2013

TFF yapata katibu mkuu wake mpya kumtangaza J4

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF)  limepata Katibu Mkuu Mpya atakayechukua nafasi iliyoachwa wazi na Angetile Osiah aliyemaliza muda wake na kukaimiwa na Afisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface Wambura.
Taarifa toka ndani ya TFF zinasema kuwa jina la mmoja kati ya waliotuma maombi ya kuiomba kazi hiyo amepatikana ila atatangazwa rasmi siku ya Jumanne.
Huyo atakuwa katibu mkuu wa kwanza katika uongozi mpya wa Rais Jamal Malinzi aliyechaguliwa Oktoba 27 mwaka huu katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika jijini Dar es Salaam. Je aliyekinyakua ajira hiyo TFF ni nani?" Tusubiri hapa hapa MICHARAZO itawaletea jina mapema kabla ya hiyo Jumanne.

No comments:

Post a Comment