STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 18, 2013

Msanii Remmy Williams anayefanya kazi Italia atua Bongo

MSANII wa mziki wa bongo fleva Remmy Williams
MSANII wa mziki wa bongo fleva Remmy Will akiwasili nchini akitokea Italy

MSANII wa mziki wa bongo fleva Remmy Will  (kushoto ) akiwasili nchini akitokea Italy kulia ni meneja wake nchini Italy Wactor Fizio walipowasili nchini Tanzania

MSANII wa mziki wa bongo fleva Remmy Williams
MSANII wa mziki wa bongo fleva Remmy Williams katikati akilakiwa na baadhi ya warembo waliojitokeza kumpokea msanii huyo

MSANII wa mziki wa bongo fleva Remmy Williams akiwa ameshikwa mkono na meneja wake wa Tanzania Mcdennis Mgatha


Na Mwandishi Wetu
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Remmy Williams anayefanya shughuli zake za muziki nchini Italia ameingia nchini jana kwa ajili ya kufanya shughuli na wasanii wenzake wa nyumbani Tanzania.
Akizungumzia ujio wake mara baada ya kutua uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam, msanii huyo aliyekuwa ameambatana na meneka wake toka Italia, alisema lengo lake ni kutaka kuona kazi za wasanii wa Tanzania zikitamba kimataifa.
"Nataka kazi za wasanii wenzangu zitambe na kuvuka mipaka ya Tanzania na kujitangaza kimataifa, naamini nitafanya nao kazi kwa ufanisi," alisema.
Remmy aliwaomba wasanii na wadau wa muziki nchini wampe ushirikiano wa kutosha kufanikisha lengo hilo ambapo akiwa nchini atarekodi kazi kwa kushirikiana na wasanii wa hapa nchini pamoja na kushirikia maonyesho mbalimbali ya pamoja.
Meneja wake wa hapa nchini, Mcdennis Mgatha, alisema Remmy amekuja pia kutambulisha nyimbo zake mpya pamoja na kutoa nyingine akishirikiana na wasanii wa Tanzania kabla ya kuanza kuzitambulisha katika maonyesho yatakayoandaliwa.

No comments:

Post a Comment