STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 13, 2014

AC Milan yazidi kudoda Seria A

Berrard Demonico
Sassuolo - AC milan
'Muuaji' Demonico Berardi (25) akishangilia bao na wachezaji wenzake walipoiangamiza AC MIlan

KLABU ya AC Milan imeendelea kuteseka kwenye Ligi Kuu ya Italia Seria A baada ya usiku wa jana kunyukwa mabao 4-3 na 'vibonde' Sassuolo iliyokuwa uwanja wake wa nyumbani.
Shujaa wa wenyeji alikuwa ni Domenico Berardi aliyefunga mabao yote manne ya Sassuola katika dakika za 15, 28, 41 na 47 na kinda huyo mwenye miaka 19 kuweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo kufunga idadi hiyo ya mabao manne katika Seria A ikiwa ni baada ya zaidi ya miaka 80 na kumweka pabaya kocha wa AC Massimiliano Allegri.
Wageni walianza kuwaduwaza wenyeji kwa kupata mabao mawili ya chapchap kupitia nyota wake, Robinho na Mario Balotelli waliofunga dakika ya 9 na 13 kabla ya Berardi kuyarejesha na kuongeza jingine na kufanya timu ziende mapumziko zikiwa 3-2.
Kipindi cha pili Berardi aliendelea kuinyanyasa ngome ya AC Milan kwa kuongeza bao jingine kabla ya wageni kujipatia bao jingine la kujifutia machozi lililofungwa na Montolivo dakika nne kabla ya kumalizika kwa mchezo huo na kuicha Milan ikisaliwa na pointi zake 22 ikiwa nafasi ya 11.
Kwa ushindi huo Sassuolo iliyokuwa nafasi ya 18 imepanda hadi kwenye nafasi ya 16 ikifikisha pointi 17.



















No comments:

Post a Comment