STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 13, 2014

Uganda The Cranes waanza vyema CHAN 2014


Man of the match Yunus Ssentamu celebrates his second goal against Burkina Faso
Sentamu akishangilia bao lake la pili

VINARA wa kandanda Kanda ya Afrika Mashariki, Uganda The Cranes imeanza vyema kampeni zake za kuwania ubingwa wa fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) baada ya kuisambaratisha Burkina Faso kwa mabao 2-1 katika pambano la kundi B lililochezwa usiku wa jana.
Mabao mawili kutoka kwa aliyekuwa nyota wa mchezo huo, Yunus Sentamu moja kila kipindi yalitosha kuiweka Uganda kileleni mwa kundi hilo ikifikisha pointi tatu na mabao mawili, huku Burkina Faso wakienda mpaka mkiani ikiwa haina pointi yoyote.
Sentamu alifunga bao la kwanza kwenye dakika ya 15 kabla ya kuongeza jingine dakika ya 73 na wapinzani wao kupata bao la kufutia machozi dakika mbili kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kupitia kwa Cyrille Bayala.
Michuano hiyo itaendelea tena jioni ya leo kwa mechi za kundi C, Ghana kuvaana na Jamhuri ya Congo na Libya kukabiliana na wawakilishi wengine wa ukanda wa CECAFA, Ethiopia.

No comments:

Post a Comment