STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Simba, KCC hapatoshi kesho Fainali Kombe la Mapinduzi

kikosi cha Simba
KCC ya Uganda
 KIVUMBI cha michuano ya Kombe la Mapinduzi kinatarajiwa kumalizika kesho kwa pambano la Fainali kati ya Simba dhidi ya KCC ya Uganda litakalochezwa jioni kwenye uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar.
Simba inaivaa KCC baada ya kuitoa nishai URA pia ya Uganda kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Mganda Joseph Owino, aliyekuwa akiichezea timu hiyo kabla ya kurejea Msimbazi na lile la Amri Kiemba.
KCC wenyewe waliwavua ubingwa Azam kwa kuwakandika mabao 3-2, licha ya kutanguliwa kufungwa 2-1 hadi wakati wa mapumziko.
Simba iliyowahi kunyakua taji hilo miaka miwili iliyopita, itakuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha Kombe hilo halichukuliwi na wageni kwani tangu ilipoanzishwa michuano hiyo taji hilo halijawahi kutoka nje ya Tanzania.
Ikiwa chini ya kocha Zdrakov Lugarosic, Simba itaendelea kuwategemea wachezaji wake nyota Ramadhani Singano, Harun Chanongo, Amri Kiemba na golini atakuwa Ivo Mapunda kuhakikisha KCC hawafuruki katika mchezo huo wa fainali unaotarajiwa kuhudhuriw ana viongozi wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wale wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikizingatiwa kesho ni mapumziko kitaifa.
KCC ambayo haikuwa ikipewa nafasi kubwa, kabla ya kuja kuongoza kundi A walilokuwa na Simba katika mechi za awali siyo timu ya kubeza kwani imetoa upinzani mkubwa ikiwa haijafungwa mchezo wowote kama wapinzani wao ambao wana nyongeza ya rekodi ya kutoruhusu bao lolote langoni mwao mpaka sasa.
Timu huyo ya Jiji la Kampala inawategemea wachezaji wake kadaa nyota kama Ibrahim Kiiza na wengine ambao waliisimamisha Azam na kuwavua taji katika mechi ya Nusu Fainali ya kwanza juzi.
Uongozi wa Simba umenukuliwa jioni hii toka Zanzibar wakisema kikosi chao kipo imara tayari kuwapa raha Wazanzibar wanaosherehekea miaka 50 ya Mapinduzi na watanzania kwa ujumla ili kulibakisha taji hilo katika ardhi ya Tanzania kwa kuwazuia KCC wasiondoke nalo kama walivyofanya dada zao wa netiboli walioifunga timu ya taifa ya Tanzania kwenye fainali pia juzi.

No comments:

Post a Comment