STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Zimbabwe yaibana Morocco CHAN 2014

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/en/8/8d/2014_African_Nations_Championship.png
TIMU ya soka ya taifa ya Zimbabwe imefanikiwa kuvuna pointi moja mbele ya Morocco baada ya kutoka nayo suluhu ya kutofungana katika pambano la kundi B la Michuano ya Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani iliyoanza jana nchini Afrika Kusini.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Athlone, mjini Cape Town lilikuwa la vuta nikuvute kwa muda wote wa dakika 90 na kushuhudiwa timu hizo zikikosa mabao ya wazi na kufanya matokeo kuwa 0-0.
Mechi nyingine ya kundi hilo inatarajiwa kuanza hivi punde kati ya Uganda The Cranes itakayoumana na Burkina Faso kwenye uwanja huo huo wa Athlone.
Kesho katika mfululizo wa michuano hiyo iliyoasisiwa mwaka 2008,  Ghana itaumana mapema na Congo kabla ya Libya kuvaana na Ethiopia katika mechi za Kundi C na mechi za raundi ya kwanza zitamalizika Jumanne kwa mechi za kundi D kati ya DR Congo dhidi ya Mauritania na Gabon kuumana na Burundi.

No comments:

Post a Comment