STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Manchester City yaiua Newcastle kwao, na kuing'oa Chelsea kileleni

Edin Dzeko akishangilia bao lake dhidi ya Newcastle



BAO la mapema lililofungwa na Edin Dzeko katika dakika ya nane na jingine la dakika za lala salama kupitia kwa Alvaro Negredo yametosha kuipaisha Manchester City hadi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England wakiiporomosha Chelsea iliyokwea nafasi hiyo jana.
City wakiwa ugenini kuifuata Newcastle United iliweza kupata mabao hayo na kuifanya ifikishe pointi 47, moja zaidi ya ilizonazo Chelsea iliyoibamiza Hull City nyumbani kwao kwa mabao 2-0.
Dzeko alifunga bao la kwanza akimalizia kazi nzuri ya beki wa pembeni wa City, Aleksandar Kalarov kabla ya Negredo kuwaduwaza wenyeji dakika za nyongeza kwa kufunga bao la pili na kuifanya City imalize mechi hiyo ikiwa vidume, ikiwa ni mechi yao ya sita mfululizo kushinda katika Ligi.
Hata hivyo vijana hao na Manuel Pelligrini wanaweza kusalia kwa muda tu kileleni hapo kama Arsena ambayo kesho itashuka dimbani itapata ushindi ugenini dhidi ya Aston Villa katika mechi pekee ya ligi hiyo.
Hivi punde pambano la Stoke City dhidi ya Liverpool litaanza kuchezwa katika mfululizo wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment