STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Afrika Kusini, Mali waanza vyema CHAN 2014

Wachezaji wa Bafana Bafana wakishangilia ushindi wao jana dhidi ya Msumbiji

TIMU ya taifa ya Nigeria jana ilianza vibaya michuano ya CHAN baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Mali huku wenyeji wa michuano hiyo inayohusisha wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika, ikipata ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Msumbiji.
Katika mechi ya wenyeji iliyochezwa uwanja wa Cape Town, jijini Cape Town, Msumbiji iliwashtua wenyeji wao kwa kupata bao la kuongoza lililofungwa kwenye dakika ya 11 kupitia Diogo.
Bao hilo lilikuja kurejeshwa na Bernard Parker katika dakika ya 30 kwa mkwaju wa penati na kufanya hadi mapumziko timu hizo kuwa nguvu sawa  kwa bao 1-1.
Kipindi cha pili kilikuwa cha wenyeji baada ya kujipatia mabao mawili kupitia kwa Hlompho Kekana na Parker kwa mara nyingine tena na kufanya Afrika Kusini kuzoa pointi tatu na kuongoza kwenye kundi lake la A ikifuatiwa na Mali waliowazabua majirani zao Nigeria kwa mabao 2-1.
Mabao ya washindi yalifungwa na Abdoulaye Sissoko katika dakika ya 11 na Adama Troure la dakika ya 54 kabla ya Nigeria kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na Fuad Salami.
Jioni hii kuna mechi nyingine mbili zinazoendelea ambako Zimbabwe na Morocco mpaka sasa hazijafunga zikikaribia kwenda mapumziko na mechi ya Uganda The Cranes na Burkina Faso itafanyika usiku na MICHARAZO itawaletea matokeo yake.

No comments:

Post a Comment