STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Juventus haikamatiki Seria A, Roma, Napoli nazo zaua Italia

TIMU ya Juventus imeendelea kujikita kileleni baada ya kupata ushindi ugenini dhidi ya Cagliari, huku Roma na Napoli nazo zikipata ushindi wa kishindo katika mechi zao za Seria A jioni ya leo.
Juventus kwa ushindi huo wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji wao imeifanya ifikishe pointi 52 na kufuatiwa na Roma  yenye 44 baada ya kushinda nyumbani mabao 4-0 dhidi ya Genoa na Napoli kushinda mabao 3-0 na kujikita nafasi ya tatu ikiwa na pointi 42.
Mechi nyingine za leo katika Seria A imeshuhudia Fiorentina ikipata sare ya 0-0 ugenini dhidi ya Torino na  Atalanta ikishinda nyumbani 2-1 dhidi ya Catania.

No comments:

Post a Comment