STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Manchester City kuiengua Chelsea kileleni itaivaa Newcastle Utd

KLABU tishio kwa sasa nchini England, Manchester City chini ya kocha Manuel Pellegrini leo ina nafasi ya kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu ya Engalnd iwapo itaishinda ugenini dhidi ya Newcastle United na kuinegua Chelsea iliyoing'oa Arsenal jana kwa kuicharaza Hull City.
City itakuwa ugenini kuvaana na Newcastle ina pointi 44 na iwapo itashinda mechi hiyo ya jioni ya leo itafikisha pointi 47, moja zaidi ya zile ilizonazo Chelsea iliyokaa kileleni na pointi 46, moja zaidi ya waliokuwa vinara Arsenal ambayo yenyewe itashuka dimbani kesho kuvaana na Aston Villa ugenini.
Kikosi cha Pellegrini ambayo kimecheza mechi 12 kuanzia Desemba Mosi na kufunga mabao 36 katika michuano yote inayoshiriki msimu huu, huku ikiwa na rekodi ya kushinda nyumbani hata hivyo hawatakuwa na kazi nyepesi kwa Newcastle watakaokuwa uwanja wao wa nyumbani wa St James Park kutokana na timu kupoteza mechi mbili mfululizo kutoka kwenye lindi la ushindi wiki chache zilizopita.
Manchester City wanapewa nafasi kubwa ya kushinda pambano hilo kutokana na kuwa na safu kali ya ushambuliaji ikiongozwa na Alvaro Negredo, Edin Dzeko na kiungo Yaya Toure Mchezaji Bora wa Afrika kwa mara ya tatu mfululizo.
Mbali na mechi hiyo inayofuatiliwa kwa ukaribu na mashabiki wa kandanda pia leo kuna mechi nyingine nzuri ya Stoke City itakayopikaribisha Liverpool kabla ya kesho kuhsuhudiwa Aston Villa kuialika Arsenal katika pambano ambalo kama The Gunners watashinda itadhihirisha dhamira yake ya kunyakua taji la Ligi msimu huu baada ya miaka mingi ya kulikisikia kwenye bomba tu.

RATIBA
Jumapili Januari 12 
17:05 Newcastle V Man City
19:10 Stoke V Liverpool
Jumatatu Januari 13 

23:00 Aston Villa V Arsenal

No comments:

Post a Comment