STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Tanzia! Nyota wa zamani wa Reli, Taifa Stars afariki


Boniface Njohole enzi za uhai wake (Picha: Mtanda Blogu)
MCHEZAJI wa zamani wa klabu ya Reli ya Morogoro na Taifa Stars, Boniface Njohole amefariki dunia katika kijiji cha Mngeta tarafa ya Ifakara wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro. 
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mkoani Morogoro Karibu Mtendaji wa chama cha soka mkoa wa Morogoro (MRFA) Hamis Semka alisema Njohole amefariki dunia katika kijiji cha Mngeta majira ya saa 5:30 asubuhi baada ya kuumwa kwa muda mrefu.
Hata hivyo taarifa zaidi zinasema kuwa Njohole aliyekuwa akifahamika kama Boni, alikuwa akisumbuliwa na matataizo ya Figo na alikuwa akitibiwa Moshi, kabla ya kurejeshwa nyumbani kwake Ifakara na kukutwa na mauti. 
Taarifa zaidi zinaendelea kufuatiliwa kujua mazishi na taratibu nyingine juu ya msiba wa mwanandinga huyo
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na wadau wote wa soka kwa msiba wa Boniface Njohole na kutakia moyo wa subira kwa kutambua kuwa Kila Nafsi Itaonja Mauti. Mungu Aiweke Roho ya Marehemu Mahali Pema. Ameen

No comments:

Post a Comment