STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 12, 2014

Liverpool yatakata, Suarez nouma!

Liverpool's Steve Gerrard scores from the spot
Gerrard akitupia kambani bao la penati la Liverpool

LUIS Suarez ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu cha Ufungaji Bora wa Ligi Kuu ya England baada ya muda mfupi uliopita kufunga mabao mawili na kufikisha mabao 22 wakati akisaidia Liverpool kupata ushindi mnono ugenini wa mabao 5-3 dhidi ya Stoke City.
Suarez alifunga mabao hayo katika dakika za 32 na 71, huku wachezaji waliokuwa majeruhi nahodha Steven Gerrard na Daniel Sturridge wakifunga bao moja moja, Gerrard akifunga kwa mkwaju wa penati, huku bao la kuongoza la Liverpool likifungwa na beki wa Stoke City, Ryan Shawcross dakika ya 5 tu ya mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Britannia.
Sturridge alifunga bao la tano dakika tatu kabla ya kumalizika kwa pambano hilo akitokea benchi, huku wenyeji wakipata mabao yao ya kufutia machozi kupitia kwa  Peter Crouch, Charlie Adam na Jonathan Walters.
Kwa ushindi huo Liverpool imefikisha jumla ya pointi 42 na kurejea kwenye nafasi ya nne ikiishusha Everton na Tottenham ambazo jana zilitakata na ushindi wa mabao mawili kila moja.

No comments:

Post a Comment