STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 13, 2014

Simba yashindwa kutamba kwa Waganda taji hilooo!


FUPA lililowashinda watetezi wa Kombe la Mapinduzi, Azam jioni ya leo umewashinda pia Simba, baada ya 'Mnyama' kuchezea kichapo cha bao 1-0 toka kwa vijana wa KCC ya Uganda ambao wamenyakua taji hilo na kuondoka nalo ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwa timu ya nje ya Tanzania kutwaa kombe hilo.
Simba ambayo ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kuficha aibu ya Tanzania kushuhusia timu zake zote zikikongotwa na wageni, ilishindwa kuhimili vishindo vya Waganda licha ya kucheza jihad hasa dakika za lala salama.
Bao pekee lililowanyong'onyesha Simba na watanzania kwa ujumla lilitumbukiwa na Herman Wasswa katika kipindi cha kwanza.
Kwa ushindi huo KCC imekuwa klabu ya kwanza nje ya Tanzania kunyakua taji hilo tangu lilipoanzishwa mwaka 2006, ikiwa haijapoteza mchezo wowote tangu kuanza kwa michuano hiyo Januari Mosi.
Timu hizo zote zilikuwa kundi B mpaka kufika fainali zilikuwa hazijapoteza mechi zao na katika mechi baina yao zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu.
Michuano hiyo ilishirikisha timu 12 nne kutoka nje na nyingine za Tanzania Bara na Zanzibar. klabu za nje ni URA na KCC za Uganda, Tusker na AFC Leopards za Kenya.
Kutwaa kwa taji hilo KCC imefuata nyayo za dada zao wa netiboli waliotwaa ubingwa wa mchezo huo kwa kuifunga Tanzania katika fainali siku mbili zilizopita.
Simba iliifunga URA ya Uganda katika mechi ya nusu fainali na KCC ikailamba Azam kwa mabao 3-2 na kuitemesha taji ililotwaa mwaka jana kwa kuichapa Tusker ya Kenya.

No comments:

Post a Comment