STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 15, 2014

Cheka aumia mkono mazoezini, pambano lake na Mrusi hatihati

Francis Cheka
Bondia Francis Cheka

BINGWA wa Ngumi za Kulipwa anayeshikilia taji la IBF-Afrika, Francis Cheka yupo katika hati hati ya kuvaana na mpinzani wake kutoka Russia Valery Brudov, baada ya kujiumiza mkono akiwa kwenye mazoezi kujiandaa na pambano hilo lililopangwa kufanyika Februari 8, jijini Dar es Salaam.
Pambano hilo limepangwa kuchezwa kwenye uikumbi wa PTA na litakuwa la uzito wa Light Heavy raundi 12 likiwa limeandaliwa na promota Juma 'Jay' Msangi.
Akizungumza naMICHARAZO mapema leo, Cheka alisema amejiumiza mkono wa kulia akiwa kwenye mazoezi na amekimbilia hospitali kuchunguzwa kutokana na anachodai kusikia maumivu makali.
Bondia huyo aliyekuwa akishikilia taji la Dunia la WBF kabla ya kunyukwa kwenye pambano la kimataifa nchini Russia Desemba 21 mwaka jana, alisema mkono huo umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu na alishautibia ukapona, ila juzi ni kama ameutonesha na kumfanya ashindwe kufanya chochote kwa maumivu.
"Nipo hospitalini kwa sasa nimekuja kuucheki mkono wangu wa kulia ambao umekuwa ukinisumbua kitambo kirefu na kupona, ila juzi nikiwa kwenye mazoezi nilijitonesha na ninasikia maumivu makali na pia nashindwa kufanya lolote," alisema.
Alipouliuzwa anadhani itakuwaje wakati pambano lake la kimataifa dhidi ya Mrusi likiwa linakaribia, Cheka alisema atatoa maamuzi baada ya kujua hali ya mkono wake, kwani alidai saa nane alitakiwa kuingia katika kliniki maalum hospitalini.
"Sijajua mpaka sasa kuhusu mustakabali wa mchezo wangu, nataka kujua kwanza hali ya mkono wangu kwa sababu bila kuwa fiti ni vigumu kupanda ulingoni," alisema Cheka ambaye pia anashikilia mataji ya ICB, UBO na WB-C.

No comments:

Post a Comment