STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 15, 2014

Yanga yaendelea kugawa dozi Uturuki

MABINGWA wa soka nchini, Yanga imeendelea kufanya vyema kwenye mazoezi yake nchini Uturuki baada ya leo kuikwanyua Altay SK kwa mabao 2-0 ikiwa ni ushindi wa pili tangu itue nchini humo kujiandaa na duru la pili la Ligi Kuu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Uturuki kupitia akaunti ya FB ya klabu hiyo maboa ya Yanga yaliwekwa kimiani katika kipindi cha pili kupitia kwa Didier Kavumbagu katika dakika ya 46 na Emmanuel Okwi kwenye dakika ya 57.
Klabu hiyo ya Antay SK inaashiriki Ligi daraja la Pili nchini humo na imekumbana na kipigo hicho baada ya ndugu zao wa Ankara Sekerspor kuchezea kipigo cha mabao 3-0 katika mechi ya kwanza kwa mabingwa hao wa Tanzania ikiwa nchini humo.
Mara baada ya mchezo huo wa leo Yanga itakamilisha ziara yake ya mafunzo wiki ijayo kwa kucheza na timu ya Simurq Zaqatala FC ya nchini Azberbaijan iliyopo katika Ligi Kuu ya nchi hiyo na msimu uliopita ikiwa imekamata nafasi ya nne kwenye msimamo wa Azerbaijan Premier League.

No comments:

Post a Comment