STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 15, 2014

Kocha John Simkoko aula TAFCA-Moro

John Simkoko
 CHAMA cha makocha wa mpira wa miguu Tanzania (TAFCA) mkoa wa Morogoro kimepata viongozi wake wapya kufuatia uchaguzi uliofanyika hivi karibuni katika uwanja wa Jamhuri, mjini humo.
Katika uchaguzi huo uliovuta hisia za makocha wa soka mkoani Morogoro, John Simkoko alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho wakati nafasi ya katibu mkuu imekwenda kwa Ahmed Mumba.
Waliochaguliwa katika nafasi tatu za wajumbe wa kamati ya utendaji ya chama hicho ni John Tamba, Rashid Amri na Nyamtimba Muga wakati Jonas Mhango akichaguliwa katika nafasi ya mweka hazina na Charles Mwakambaya akiibuka mshindi katika nafasi ya mjumbe wa mkutano mkuu.
Awali, akizungumza kabla ya uchaguzi huo, mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Morogoro (MRFA), Pascal Kihanga ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi aliwataka makocha mkoani Morogoro kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwao kwa lengo la kuhakikisha mchezo wa soka unapiga hatua kubwa mkoani hapa.
Naye, Simkoko akizungumza baada ya uchaguzi, alisema amejipanga vizuri kukiongoza chama hicho na kwamba watatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

No comments:

Post a Comment