STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 15, 2014

Bafana Bafana yabanwa na Mali CHAN 2014

http://www.citypress.co.za/wp-content/uploads/2013/06/bafana-bafana.jpg
WENYEJI Afrika Kusini pamoja na kutangulia kupata bao la mapema kwenye kipindi cha kwanza kwa mkwaju wa penati, imeshindwa kuendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Mali.
Bafana Bafana ilipata bao lake kwenye dakika ya 25 kupitia kwa mshambuliaji wake nyota Benard Parkers ambalo lilikuwa la tatu katika mashindano hayo baada ya Mali kucheza madhambi langoni mwao.
Bao hilo lilidumu hadi mapumziko kabla ya kipindi cha pili kuanza na Mali kuonyesha uhai kwa kushambulia lango la Bafana Bafana na kufanikiwa kupata bao la kusawazisha kupitia kwa Ibourahima Sidide katika dakika ya 51.
Kwa matokeo hayo Afrika Kusini wameendelea kuongoza kundi hilo ikiwa na pointi nne sawa na Mali ila zinatofautiana kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa, Bafana Bafana wakiwa na mabao manne na kufungwa mawili, huku Mali ikiwa na matatu ikiruhusu mawili.
Mechi nyingine ya kundi hilo inatarajiwa kuchezwa muda mchache baadaye kwa Nigeria kuumana na 'Mambaz' ya Msumbiji katika pambano linalotarajiwa kuwa kali kutokana na ukweli timu zote zilipokea vipigo katika mechi zao za fungua dimba ya CHAN 2014.

No comments:

Post a Comment