STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 15, 2014

Nigeria yaifumua Msumbiji 4-2, Uganda kesho

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj4pAFgBXFCrZ5aG231HuhM0mTIqT7jzK-NSYgSVzDX6C3Mg2gM-XUOtN_y-TnzmVGhcytRh8sDaMUXLZ1zcAoFw0wTLTRch31uj8OAuHh-N_L7__zWnYui1ewNtDBlLTTdIsTPgoWMEVpr/s640/Nigeria+CHAN+match.jpg
NIGERIA imezinduka kwenye michuano ya CHAN baada ya kuikandika Msumbiji mabao 4-2 ktika pambano la raundi ya pili kwa timu za kundi A lililochezwa usiku huu.
Msumbiji waliofungwa mabao 3-1 na wenyeji Afrika Kusini, walianza kupata bao dakika ya 10 ya mchezo huo kupitia kwa Dario Khan, lililodumu kwa dakika moja kabla ya Ede kurejesha akimaliza kazi ya Egwuekwe.
Nigeria iliongeza bao la pili dakika ya 13 kupitia kwa Rabiu Ali kabla ya Msumbiji kuchomoa dakika saba baadaye kupitia Diogo na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 2-2.
Kipindi cha pili kilianza kwa Nigeria kujipatai bao la tatu kwa mkwaju wa penati kupitia kwa Ali tena kwenye dakika ya 54 na dakika mbili kabla ya pambano hilo kumalizika Imenger aliiongezea Nigeria bao la nne lililowapa ushindi wao wa kwanza kwenye mchuano hiyo.
Michuano hiyo inaendelea tena kwa michezo ya kundi B ambapo Uganda itaumana na Zimbabwe mapema kabla ya Burkina Faso kuumana na Morocco usiku. Katika mechi za awali Uganda iliichapa Burkinabe mabao 2-1 na Morocco na Zimbabwe zilitoshana nguvu kwa kutofunagana.

No comments:

Post a Comment