STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 4, 2014

Chelsea yaipa nafuu Arsenal, yaitungua Man City kwao

BAO pekee lililofungwa dakika ya 32 na Ivanovic usiku wa jana limeisaidia Chelsea kuibuka na ushindi ugenini mbele ya Manchester City na kuipa nafuu Arsenal waliopo kileleni.
Man City ambayo ipo kwenye kiwango cha hali ya juu na iliyokuwa ikigawa dozi nene kwa wapinzani wao, ilishindwa kuamini kama imelala kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Etihad baada ya pambano hilo kumalizika.
Hata hivyo katika mchezo wa jana ilidhibitiwa na vijana wa Jose Mourinho na kuambulia kipigo cha kwanza baada ya mechi  20 mfululizo bila kupoteza na cha kwanza tangu walipofungwa Novemba mwaka jana na Sunderland.
Kwa ushindi huo wa jana Chelsea wamefikisha pointi 53 sawa na Man City na kutofautishwa na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Kileleni ameendelea kusalia Arsenal ambayo ni wazi jana ilikuwa ikiangusha dua mbaya kwa City ili wasishindi mchezo huo na kuwatoa kwenye uongozi, dua lililojibu kwa Chelsea kuwaziba mdomo vijana wa Etihad.

No comments:

Post a Comment