STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 2, 2014

David Naftal afichua siri adai , soka la Bongo limejaa fedha bila mikakati

David Naftal
KIUNGO mkabaji wa zamani wa klabu ya Simba anayecheza soka la kulipwa nchini Kenya, David Naftal amesema soka la Tanzania limejaa fedha, lakini linazidiwa umahiri katika uendeshaji wa klabu na majirani zao wa Kenya.
Naftal alisema kutokana na soka la Tanzania kuwa fedha nje nje, imewafanya wachezaji wengi wa kigeni kupigana vikumbo kuja nchini hata wale ambao viwango vyao siyo vya kuridhisha kwa vile hupapatikiwa na wenyeji wao.
Akizungumza na MICHARAZO toka Kenya, kiungo huyo aliyewahi kuichezea pia AFC Arusha, alisema klabu za Kenya zipo makini katika uendeshaji wa shughuli zake na mipango mkakati ya kukuza soka la Kenya tofauti na Tanzania ambazo 'siasa' zimezidi kiasi cha kufanya soa lake lidumae kwa miaka mingi.
Naftal alisema viongozi wa klabu za Kenya ni weredi na makini katika kuendesha shughuli zao na wanathamini sana wachezaji na ni nadra kusikia wakiwatuhumu wachezaji kufanya hujuma kama ilivyo Tanzania.
"Huku viongozi wapo makini na kazi zao na wanathamini wachezaji, huwezi kusikia kiongozi akimtuhumu mchezaji kufanya hujuma timu zinapopata matokeo kwa kutambua soka ndivyo lilivyo, tofauti na huko Tanzania," alisema.
Hata hivyo alisema soka la Kenya halina fedha nyingi kama Tanzania ambapo imekuwa mvuto wa wanasoka wa nchi mbalimbali kukimbilia.
"Kwa kweli kuna tofauti kubwa ya mfumo wa soka wa Kenya na Tanzania, wenzetu hapa wapo makini katika kupanga mikakati ya kuinua timu zao na soka lao kwa ujumla tofauti na Tanzania, japo hawana fedha nyingi kamka ilivyo huko nyumbani Tanzania," alisema.
"Kutokana na fedha kuwa za kumwaga Tanzania na wadau wake kuwa wepesi kumwaga mamilioni, imefanya wachezaji wengi wa nje kupenda kuja kucheza Tanzania hata kama hawana viwango vikubwa kama wazawa," aliongeza.
Naftal aliongeza kutokana na tofauti aliyoiona Kenya tangu alipotua nchini humo kuichezea Bandari ya Mombasa inayoshiriki Ligi Kuu, imemfanya kukosa hamu ya kutaka kurudi Tanzania badala yake azidi kusonga mbele

No comments:

Post a Comment