STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 7, 2014

Manchester United wawakumbuka wenzao waliokufa kwa ndege 1958

Forever there: United have a poignant memorial wall for supporters to always go and visitKLABU ya Manchester United leo inatarajia kuwakumbuka watu 23 ambao walipoteza maisha katika ajali ya ndege jijini Munich Februari 6 mwaka 1958. Wachezaji nane wa United na viongozi watatu ni miongoni mwa waliokufa wakati ndege iliyowabeba wachezaji wa timu hiyo kutoka katika mchezo wa Kombe la Ulaya jijini Belgrade kushindwa kupaa. Ndege hiyo ilitua jijini Munich kwa ajili ya kuongeza mafuta na baada ya kushindwa kuruka mara mbili ndege hiyo ilipata ajali wakati ikijaribu tena kuruka kwa mara ya tatu. Watu 21 walifariki katika eneo la tukio huku rubani wake Kenneth Rayment alifariki wiki tatu baadae na Duncan Edwards ambaye anahesabika kuwa mmoja wa wachezaji nyota kabisa wa Uingereza yeye alifia hospitali siku 15 baadae. Turnout: As always, a large group of fans were there on the anniversaryGolikipa wa United Harry Gregg yeye alifanikiwa kutoka salama lakini alirejea katika eneo la tukio kujaribu kuwaokoa majeruhi katika sehemu salama. Wachezaji wawili Johnny Berry na Jackie Blanchflower wote walishindwa kucheza soka tena kutokana na majeraha ya ajali hiyo.Mashabiki wa United
Remembered: Sir Bobby Charlton and Gary Neville were among those who made their way to Old Trafford
Sir Bobby Charlton na Gary Neville walifika Old Trafford

No comments:

Post a Comment