STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 7, 2014

UNAJUA MADHARA YA KUSIKILIZA SIMU KWA MUDA MREFU?


TANGU teknolojia ya Simu za Mkononi kuingia nchini, Watanzania wamekuwa kama waliowehuka na kifaa hicha cha mawasiliano ya kisasa.
Iwe kwenye daladala, vijiweni na hata majumbani na ofisini tymekuwa tukishuhudia ndugu, jamaa na rafiki zetu na penginee wewe mwenyewe msomaji unatumia muda mrefu kusikiliza au kuongea na simu dhidi ya unawapigia au wanaokupigia.
Je umeshawahi kujiuliza madhara yanayotokana na kusikiliza au kuongea kwa muda mrefu na simu? 
Ebu shuka na taarifa hii ujue namna gani tunavyohatarisha maisha yetu bila kujua au kule kusumbuliwa na ulimbukeni wa teknolojia hii mpya ambayo imekuwa ikiwazuzua watu wengi bila kujali rika, jinsia au nafasi yao ndani ya jamii.

Leo tutaangalia jambo la ajabu kidogo na kama unabisha utajaribu mwenyewe kisha utajionea. Matumizi ya Simu za kiganjani yameongezeka sana ndani na nje ya nchi. 


Simu hizi licha ya kuwa na msaada mkubwa katika maendeleo ya jamii pia zina mambo yake ambayo yanashangaza na kutisha kidogo/sana!!!! 

Leo nitawaelekeza namna ya kupika yai kwa kutumia simu mbili za mkononi. 
Baada ya somo hili jaribu kufanya jaribio na ujionee mwenyewe. Mahitaji: Simu mbili za kiganjani, Glasi/Bilauri ya maji na Yai ambalo halijapikwa wala kuvunjika. 
Yai likiwa limeelekezewa simu mbili zilizounganishwa kwa mawasiliano

Hatua: Chukua simu ya kwanza na upige kwenda namba ya simu yapili, pokea simu ya pili na kuiacha hewani kisha chukua glasi yenye yai na uiweke kati ya simu hizo mbili kwa dakika 65, ni vema ukajiunga na vifurushi ili usiingie gharama kubwa. 
Angalia mfano katika picha hii hapa chini. 

Baada ya dakika 65 yai litakuwa limeiva kabisa kama limechemshwa vile, Sikushauri ule yai hilo kwakuwa sijafanya utafiti wa kutosha endapo kuna madhara yoyote mtu akila au la. 
Sasa chakujiuliza hapo ndugu zangu ni je, endapo mionzi hii ya simu inaweza kuivisha protein iliyopo katika yai vipi kuhusu ubongo wako, hasa kwa wale watumiaji wakubwa wa simu!! 

Source:Kijiwe cha Wasomi

Original from: http://googlehabari.blogspot.com/2014/02/yajue-madhara-ya-kuongea-na-simu-kwa.html
Copyright EXEIdeas - All Rights Reserved

No comments:

Post a Comment