STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 7, 2014

Twiga Stas yahamishia kambi Dar

TIMU ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanawake (Twiga Stars) imehamishia kambi yake jijini Dar es Salaam kutoka Mlandizi mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya michuano ya Afrika (AWC) dhidi ya Zambia.

Kikosi hicho chini ya Kocha Rogasian Kaijage kimepiga kambi katika hosteli ya Msimbazi Center kikiwa na wachezaji 25 kutoka 30 ambao kilianza nao katika kambi ya Mlandizi mkoani Pwani.

Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya kwanza dhidi ya Zambia itachezwa Februari 14 kwenye Uwanja wa Nkoloma jijini Lusaka. Timu zitarudiana wiki mbili baadaye jijini Dar es Salaam.

Wachezaji waliopo katika kikosi hicho ni Amina Ally, Amisa Athuman, Anastasia Anthony, Asha Rashid, Esther Chabruma, Eto Mlenzi, Evelyn Sekikubo, Fatuma Bashiri, Fatuma Hassan, Fatuma Issa, Fatuma Mustafa na Fatuma Omari.

Wengine ni Flora Kayanda, Happiness Hezron, Maimuna Said, Mwajuma Abdallah, Mwapewa Mtumwa, Najiat Abbas, Pulkeria Charaji, Shelder Boniface, Sophia Mwasikili, Therese Yona, Vumilia Maarifa, Winfrida Daniel na Zena Khamis.

No comments:

Post a Comment