STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 7, 2014

Jack Wilshere awatuliza mashabiki wa Arsenal

JACK Wilshere amewapoza mashabiki wake baada ya vipimo kwenye mguu wake kuonyesha kwamba hana tatizo kufuatia mechi ya kirafiki ya England waliyoshinda 1-0 dhidi ya Denmark juzi.
Kiungo huyo wa Arsenal, aliachwa amelala chini kwenye uwanja wa Wembley kufuatia kuchezewa vibaya na Daniel Agger tukio lililolazimisgha mchezo kusimama wakati akihitaji matibabu.
Wilshere aliendelea kucheza baadaye kabla ya kutoka na nafasi yake kuchukuliwa na Adam Lallana muda mfupi kabla ya dakika ya 60. Kiungo huyo (22) haraka aliwapoza mashabiki wake waliohofu kwamba huenda ameumizwa vibaya kufuatia kuvaana na beki huyo wa Liverpool.
"Niko poa," alisisitiza kwa Sky Sports. "Panauma kidogo lakini ni mchubuko tu. Nimefanyiwa vipimo na tayari imeonyesha ni mchubuko tu hivyo itakuwa poa."

No comments:

Post a Comment