STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 10, 2014

Noma! Ronaldo ndiye mchezaji tajiri duniani

NYOTA wa Ureno anayeichezea Real Madrid, Cristiano Ronaldo ndiye mwanasoka tajiri kuliko wote duniani.
Kwa mujibu wa mtandao wa Goal.com, nahodha huyo watimu ya taifa ya Ureno ndiye kinara katika orodha hiyo iliyotangazwa leo.
Mkali huyo amerithi nafasi hiyo ya kwanza iliyokuwa ikishikiliwa na David Beckham kwa muda mrefu kabla hajastaafu soka msimu uliopita. 
Ronaldo ambaye alisaini mkataba mnono zaidi na Real Madrid miezi kadhaa iliyopita amempita mshindani wake Lionel Messi na mwanasoka anayelipwa zaidi kimshahara Wayne Rooney.
Samuel Eto'o ndiye Mwaafrika pekee aliyeingia kwenye listi ya wanasoka matajiri zaidi duniani.
Hii ndiyo orodha kamili:
1. Cristiano Ronaldo £122m
2. Lionel Messi £120.5m
3. Samuel Eto'o £70m
4. Wayne Rooney £69m
5. Kaka £67.5m
6. The Neymar family £66m
7. Ronaldinho £64m
8. Zlatan Ibrahimovic £57m
9. Gianluigi Buffon £52m
10.Thierry Henry £47m
SOURCE: Goal.

No comments:

Post a Comment