STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 10, 2014

Ronaldo azidi kuipaisha Real Madrid

High flying: Cristiano Ronaldo hurdles Levante's goalkeeper Keylor Navas
Ronaldo akiwajibika uwanjani
MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo usiku wa jana alisaidia timu yake kuzidi kujichimbia kileleni baada ya kufunga moja ya mabao yaliyoisaidia Madrid kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Levante.
Real Madrid imefikisha pointi 67 na kuwakimbia Atletico Madrid wenye pointi 64 timu zote zikiwa zimecheza mechi 29.
Ronaldo alifunga bao hilo katika dakika ya 11 akiunganisha kona ya Angel Di Maria kabla ya kumtengenezea pande zote Marcelo aliyefunga bao la pili.
Bao la tatu la vinara hao lilitiwa kimiani na Karabellas dakika ya 81.
Katika mchezo huo Levente walipata pigo baada ya David Navarro kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kosa la kumchezea vibaya Ronaldo katika dakika ya 49.
Barcelona ambayo juzi ilikandikwa na vibonde Real Valledolid ipo katia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 63 na kutishia amani utetezi wa taji lake la La Liga msimu huu.

No comments:

Post a Comment