STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 3, 2014

Pambano la Simba, Ruvu laingiza Mil 20

PAMBANO la Ligi Kuu ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Ruvu Shooting iliyochezwa jana (Machi 2 mwaka huu) imeingiza sh. 20,610,000 ambapo kila klabu ilipata mgawo wa sh. 4,402,492 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 3,143,898.31.
Katika mchezo huo Simba iliweza kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 na kuendelea kusalia kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Azam yenye pointi 40 na kufuatiwa na Yanga yenye 38 kisha Mbeya City inayokamata nafasi ya tatu ikiwa na pointi 36.
Katika hatua nyingine mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kati ya Mlale JKT na Lipuli iliyokuwa ichezwe Machi 9 mwaka huu Uwanja wa Majimaji mjini Songea sasa itachezwa Machi 5 mwaka huu.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imefanya mabadiliko hayo ili kuipunguzia gharama timu ya Lipuli ya Iringa ambayo jana (Machi 2 mwaka huu) ilicheza mechi mjini Songea dhidi ya Majimaji.


No comments:

Post a Comment