STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 3, 2014

Kumekucha Sikinde ebu sikia vibao vyao vipya

Baadhi ya waimbaji wa Sikinde
Baadhi wa wapuliza ala za upepo, Hamis Mirambo na Mbaraka Othman
BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Wana Sikinde Ngoma ya Ukae' imekamilisha vibao vyake vitatu vipya kwa ajili ya albamu yao mpya ya 'Jinamizi la Talaka'.
Kibao cha kwanza cha Jinamizi la Talaka baadhi yenu mmeshaushikia katika vituo vya redio kwa vile ulirekodiwa toka mwaka jana, lakini vingine viwili vya Mkwezi na Deni Nitalipa mtakuwa hamjavisikia.
Wala usichokechungulia hapa mtandao wao wa https://www.hulkshare.com/sikinde, ambapo unaweza kuzisikiliza Online na kutoa maoni ama ushauri ili kuboresha ama kufanyia marekebisho nyimbo hizo kabla ya kuzinduliwa rasmi wakati wa kuadhimisha miaka 36 tangu kuanzishwa kwake.

No comments:

Post a Comment