STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 3, 2014

Yanga kuivaa Al Ahly Cairo bila mashabiki

MAMLAKA za usalama nchini Egypt katika jiji la Cairo zimewaonya mashabiki wa Al Ahly kutoingia katika uwanja Cairo kuhudhuria mechi ya raundi ya pili ya CAF Champions league kati ya Al Ahly dhidi ya Young Africans S.C.  itakayochezwa mnamo March 9.
Katika taarifa iliyotolewa jana Jumapili, polisi wa Cairo walisema kwamba itapambana na jaribio lolote la mashabiki kujaribu kuingia uwanjani.

Azmi Megahed, msemaji wa FA ya Misri, alisema raia hawatoruhusiwa kuhudhuria mechi hiyo kutoka sababu za kiusalama.

Jumamosi wiki iliyopita, polisi walipambana na mashabiki wa Zamalek White Knights ambao walijaribu kuingia katika uwanja wa Cairo kuangalia mchezo kati ya Zamalek dhidi ya mabingwa wa Angola Cabo Schrob. Fujo hizo zilipelekea kwa kukamatwa kwa mashabiki 33.
SHAFIH DAUDA

No comments:

Post a Comment