STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 4, 2014

Steve Nyerere aja na Snake Kingdom

Hii ndiyo kazi mpya ya Steve Nyerere itakayosambazwa na Proin Promotions
MWENYEKITI wa Bongo Movie Unity (BMU), Steven Mengele 'Steve Nyerere' anajiandaa kuiachia hadharani filamu yake mpya kwa mwaka 2014 iitwayo 'Snake Kingdom'.
Akizungumza na MICHARAZO, Steve Nyerere alisema filamu hiyo ya kijamii ameigiza na wakali wenzake kama Chuchu Hans, Mayasa Mrisho, Cathy Rupia, Bi Terry 'Mama Nyamayao' na wengine.
Steve Nyerere alisema filamu hiyo ni ya aina yake na kuwataka mashabiki kujiandaa kupata uhondo mara itakapoachiwa mtaani hivi karibuni chini ya kampuni mpya na inayokuja kwa kasi katika kusambaza kazi za wasanii wa filamu nchini ya Proin Promotions.
Mchekeshaji huyo anayeigiza sauti za viongozi mashuhuri, alisema 'Snake Kingdom' ni filamu iliyozalishwa na kampuni yake iliyowahi kutoa filamu kama 'Mwalimu Nyerere', 'My President', 'My Son', 'Mke Mwema' na nyingine.

No comments:

Post a Comment