STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 4, 2014

Barcelona yafungiwa kusajili Ulaya

http://www.smckorea.com/2011/fcbarcelonalaligachamps_580693_92772.jpgKLABU ya Barcelona imefungiwa kusajili wachezaji kwa vipindi viwili vya usajili na Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kukiuka taratibu za kimataifa zinazohusu usajili wa wachezaji chini ya umri wa miaka 18. 
Hatua hiyo imekuja kufuatia uchunguzi wa awali uliofanywa na shirikisho hilo kupitia mfumo wake wa uhamisho-TMS kwa mwaka uliopita. 
Barcelona wamekutwa wamekiuka vifungu kadhaa kuhusiana na uhamisho wa kimataifa sambamba na usajili wa wachezaji walio chini ya umri ambao sio raia wa Hispania. 
Uchunguzi huo ulihusisha wachezaji kadhaa walio chini ya umri huo ambao waliandikishwa na kushiriki mashindano wakiwa na timu hiyo katika kipindi cha mwaka 2009-2013.

No comments:

Post a Comment