STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 4, 2014

Wareno, Juve, Basel zashinda Europa League

http://s2.djyimg.com/n3/eet-content/uploads/2014/04/482339519.jpg
Hekaheka kati ya Juve na Lyon jana Ufaransa
http://s2.djyimg.com/n3/eet-content/uploads/2014/04/482339873.jpg
Porto walipoitoa nishai Sevilla jana kwenye Europa League

http://www.beinsports.tv/di/library/bein_us/84/42/basel-vs-valencia_1qsqz6tdnrifu10v28x9wkvfpa.jpg?t=696372997&w=830&h=466&quality=50&cropTo=top
Basel walipoikongota Valencia 3-0
http://www.uefa.com/MultimediaFiles/Photo/competitions/Comp_Matches/02/08/39/76/2083976_w2.jpg
Tevez akionyechanja mbuga kusaka bao kwa Juventus
BAO lililofungwa na Leonardo Bonucci dakika sita kabla ya pambano kumalizika limeisaidia Juventus kupata ushindi mwembamba ugenini dhidi ya Olympique Lyon ya Ufaransa katika mechi ya robo fainali ya kwanza wa Kombe la Europa League.
Ushindi huo wa ugenini umeifanya Juve kuwa na kazi rahisi kwa mechi yao ya marudiano Alhamis ijayo mjini Turin katika kujihakikisha kutinga nusu fainali ya michuano hiyo.
Katika mechi nyingine za mkondo wa kwanza za robo fainali Basel ya Uswisi iliifumua Valencia ya Hispania mabao 3-0 na kunusa nusu fainali, huku Sevilla ikinyukwa ugenini na Porto ya Ureno na Benfica ikishinda ugenini 1-0 dhidi ya AZ ya Uholanzi.
Mabao ya Basel katika mchezo hio yalifungwa na Matias Delgado aliyefunga mawili dakika ya 34 na 38 na jingine kupitia kwa Valentin Stocker dakika za lala salama.
Timu hizo zitarudiana wiki ijayo kujua timu nne za kucheza nusu fainali ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa ngazi ya klabu barani Ulaya baada ya Ligi ya Mabingwa ambayo nayo ipo hatua ya robo fainali kwa sasa.

No comments:

Post a Comment