STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 3, 2014

Younes Kaboul aikana Arsenal

http://www.myfootballfacts.com/4047.jpg
Beki Younes Kaboul anayevumishiwa kutaka kutimkia kwa mahasimu wao Arsenal
BEKI mahiri wa klabu ya Tottenham Hotspurs, Younes Kaboul amesisitiza kuwa tetesi za yeye kuhamia Arsenal sio za ukweli kwa asilimia 100. 
Mapema jana gazeti la Daily Star la Uingereza liliripoti kuwa Kaboul amewaambia marafiki zake anataka kujiunga na Arsenal wakati mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu. 
Lakini beki huyo aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa hana mpango huo kama ilivyoelezwa na gazeti hilo. 
Kaboul anaonekana kujitetea yasije kumkuta yaliyomkuta Sol Campbell mwaka 2001 ambaye alikataa kusaini mkataba mpya na Spurs na badala yake kuichagua Arsenal hatua ambayo ilipelekea kuchukukiwa na mashabiki wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment