STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 3, 2014

Taribo West aitabiria Nigeria kuizima Argentina

http://deeksobserver.com/wp-content/uploads/2013/02/taribo.jpg
Taribo West enzi akiichezea Nigeria
BEKI wa zamani wa kimataifa wa Nigeria,Taribo West, ameitabiria timu ya taifa ya Nigeria Green Eagles kuwa itapata ushindi dhidi ya Argentina.
Tai hao wa Kijani watacheza mechi hiyo dhidi ya Albiceleste huko Brazil wakati wa Kiangazi katika michuano ya kombe la Dunia. 
Nyota huyo wa zamani, anasema kwa sasa siyo tu kuwafunga bali kusonga mbele huko Rio 2014 katika Fainali hizo za Dunia .
“Kama tumefungwa mara mbili lazima tuwe na aibu ,Nina aamini tumejifunza kutokana na uzoefu. Mara mwisho tulicheza na  Argentina  2010 katika Kombe la Dunia Afrika Kusini." alisema na kuongeza;
"Hata benchi lote linaelewa hali iliyo, mechi dhidi ya Argentina wakati huu itakuwa Bora Kwetu itakuwa Bora ,” West aliuambia mtandao Goal.
Nigeria wamekuwa hawana bahati dhidi  Albiceleste Tumeshindwa katika safari tatu za Kombe la Dunia  1994, 2002 na 2010. 
Lakini West anaamini kuwa timu yake itafanya vizuri huko  Brazil.

No comments:

Post a Comment