STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 28, 2014

Yaya Toure azidi kuleta utata Manchester City

MUSTAKABALI wa kiungo mahiri wa Manchester City, Yaya Toure kusalia katika klabu hiyo imezidi kuleta utata.
Kiungo huyo amesema itakuwa heshima kwake kuichezea Paris Saint-Germain-PSG na kukuza uvumi juu ya mustakabali wake na klabu hiyo. 
Wakala wa mchezaji huyo wiki iliyopita alisisitiza mteja wake hakufurahishwa na mabingwa hao wa Ligi Kuu nchini Uingereza baada ya kueleza kusononeshwa kwake na jinsi klabu hiyo ilivyoshindwa kumpa pongezi katika siku yake ya kuzaliwa. 
Toure aliunga mkono madai hayo na kubainisha atatoa taarifa rasmi kuhusiana na mustakabali wake baada ya Kombe la dunia na sasa amedokeza kuwa na nia ya kujiunga na PSG ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu nchini Ufaransa. 
Nyota huyo amesema kwa jinsi PSG walivyojijenga na kuwa na nguvu barani Ulaya itakuwa heshima kwake kuwa sehemu ya timu hiyo siku moja kama wataona anafaa. 
Toure amekuwa mchezaji muhimu kwa City msimu huu akiwa amefunga mabao 20 katika ligi na kusaidia mengine tisa na kuifanya timu hiyo kunyakuwa taji la Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment