STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, May 28, 2014

Kipre Tchetche, Casillas, Mwmbusi ndiye Bora Tanzania 2013-2014

Kipa Hussen Sharrif 'Casillas' akiwajibika uwanjani

KIipre Tchetche
MSHAMBULIAJI nyota wa Azam, Kipre Tchetche na kipa Hussein Sharrif 'Casillas' wamefanikiwa kushinda tuzo za Wachezaji Bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliyoisha.
Tuzo hizo zilitolewa usiku wa kuamkia leo ambapo Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi alinyakua tuzo ya Kocha Bora msimu wa 2013/2014.
Casillas anayeichezea Mtibwa Sugar alishinda tuzo ya Kipa Bora, huku Tchetche akinyakua tuzo ya Mchezaji Bora na Amissi Tambwe akiwa Mfungaji Bora.
Wachezaji wote hao kila mmoja alizawadiwa kitita cha Sh. Mil. 5.2.

Zawadi nyingine zilizotolewa ni pamoja na Sh. Mil. 75 iliyokwenda kwa Azam waliotwaa ubingwa, Yanga walizoa Sh. Mil. 35, huku Mbeya City ikitwaa Sh. Mil. 26 na Simba waliokuwa wa nne walitwaa Sh. Mil. 21.

No comments:

Post a Comment