STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

AC Milan kumtema Seedorf, Pipo kumrithi

Clarence Seedorf
KLABU ya AC Milan imedaiwa inajiandaa kumtimua kazi Kocha wake wa sasa Clarence Seedorf na nafasi yake huenda ikachukuliwa na kocha wa timu ya vijana na nyota wa zamani wa klabu hiyo na timu ya taifa ya Italia (Azzurri) Filippo Inzaghi.
Kwa mujibu wa taarifa kutuka Italia zinasema kuwa, Seedorf aliyeinoa timu hiyo kwa muda wa miezi minne tu kati ya mkataba wake wa miaka miwili na nusu atafungashiwa virago kwa nia ya kuimarisha klabu hiyo imekuwa na msimu mbaya siku za karibuni kabla ya Mholanzi huyo kuisaidia kuindoa maeneo ya mkiani mwa Ligi Kuu ya nchi hiyo, Seria A.
Seedorf, 38, aliyeitumikia klabu hiyo kwa miaka 10 alipewa jukumu la kuinoa timu hiyo Januari mwaka huu kuchukua nafasi ya Massimiliano Allegri aliyefurushwa baada ya mkataba wake kusitishwa kutokana na mwenendo mbaya wa timu katika michuano iliyokuwa ikishiriki.
Pamoja na klutokuwa kocha mzoefu Mholanzi huyo aliiwezesha timu hiyo kushinda mechi 11 kati ya 19 ilizocheza Milan na kumaliza kwenye nafasi ya nane, tofauti na mtangulizi wake aliyeshinda mechi tano tu kati ya 19 za duru la kwanza.
Hata hivyo timu hiyo inayomilikiwa na Waziri Mkuu wa zamani wa Italia, Silvio Berluscoini imekwama kushiriki hata michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya kutokana na kuangushwa na pointi moja tu, hali iliyowafanya wamiliki wake kutaka kuipanga upya mabingwa hao wa zamani wa Ulaya kurejesha hadhi yake msimu ujao.
.

No comments:

Post a Comment