STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

10 kuwania taji la Miss B'moyo 2014, Mapacha Wa3 kunogesha

Washindi wa Miss Bagamoyo kwa mwaka jana wakiwa katika pozi
BENDI ya muziki wa dansi ya Mapacha Watatu wanatarajiwa kuwasindikiza warembo 10 watakaokuwa wakiwania taji la urembo la wilaya ya Bagamoyo 'Miss Bagamoyo 2014' katika shindano litakalofanyika siku ya Jumamosi wilayani humo.
Mratibu wa shindano hilo, Awetu Salim, Mkuregenzi wa Asilia Decoration, aliliambia MICHARAZO
kuwa, shindano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa hoteli Palme Tree Village wilayani humo na maandalizi yote yamekamilika na warembo wanaendelea na kambi yao mjini humo kujiandaa na mchuano huo.
Awetu alisema warembo hao watakaosindikizwa na burudani toka bendi ya Mapacha Watatu chini ya Khaleed Chuma 'Chokoraa' na Jose Mara watachuana kurithi taji hilo linaloshikiliwa kwa sasa na Elizabeth Pertty aliyetwaa katika shindano la mwaka jana (2013).
Mratibu huyo aliwataja warembo watakaochuana hiyo Jumamosi kwa jina moja moja kuwa ni; Faith, Dora, Glory, Susan, Khadija, Princess, Nkyali, Manka, Amina na Zena.
"Shindano la Miss Bagamoyo 2014 litafanyika siku ya Jumamosi ya Mei 31 jumla ya warembo 10 watachuana kuwania taji hilo na nafasi za ushiriki wa michuano ya Miss Pwani 2014, tayari tumefanikiwa kupata wadhamini kadhaa baadhi ni Chama cha Wavuvi wilaya ya Ukerewe, Duran Sound, Palme Tree Village, D'z Restaurant and Take Away," alisema Awetu.
Awetu alisema warembo watatu wa kwanza licha ya kupata zawadi, lakini wataingia kwenye kinyang'anyiro cha kushiriki shindano la Miss Pwani litakalofanyika baadaye mwaka huu.

No comments:

Post a Comment