STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

Video ya Shaa yakamilika

VIDEO ya staa wa zamani wa kundi la WAKILISHA, Sarah Kais 'Shaa' iitwayo 'Subira' imekamilika na wakati wowote itaanza kurushwa hewani.
Meneja wa msanii huyo, Said Fella alisema video hiyo iliyorekodiwa na kampuni ya Visual Lab, chini ya Adam Juma imekamilika na kwa sasa wapo katika hatua ya mwisho ya kuanza kuisambaza tayari kwa kurushwa hewani.
Alisema video hiyo imepigwa katika maeneo mbalimbali ya jijini Dar es Salaam na haitofautiani sana na ile ya 'Sugua Gaga' ambayho imemweka matawi ya juu msanii huyo.
"Video imekamilika kupigwa picha kwa sasa inarekebishwa kidogo kabla ya kuanza kusambazwa na mashabiki wa Shaa wajiandae kupata burudani zaidi na ile ya 'Sugua Gaga'," alisema.
Aliongeza, kukamilika kwa video ya wimbo huo ni mwanzo wa maandalizi ya kazi nyingine mpya za msanii huyo aliyekuwa mmoja wa washiriki na mshindi wa shindano la Coca Cola Pop Star lililofanyika mwanzoni mwa miaka ya 2000 na yeye Witness na Langa Kileo (marehemu) waliibuka kidedea kwa Tanzania na kwenda kuchuana na wasanii wenzao wa makundi ya nchi za Kenya na Uganda.

No comments:

Post a Comment