STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

Stars, Malawi kupepetana leo Taifa, kiingilio buku 5

TIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars jioni ya leo inatarajiwa kushuka dimbani kurudiana na The Flames ya Malawi katika mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni.


Stars na Malawi zinavaana leo ikiwa ni wiki moja na ushei tangu zilipoppetana mjini Mbeya na kushindwa kutambiana zikijiandaa na mechi zao za kuwania kufuzu Fainali za Afrika za mwaka 2015 zitakazofanyika nchini Morocco.
Stars iliyopiga kambi yake Tukuyu mkoani Mbeya imewasili jijini Dar es Salaam  saa 4 asubuhi kwa ndege ya Air Tanzania tayari kwa mechi hiyo kujiandaa na mechi yao ya marudiano dhidi ya Zimbambwe itakayochezwa wikiendi hii mjini Harare.


Kiingilio katika mechi hiyo kitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa upande wa VIP B na C kiingilio kitakuwa sh. 10,000 wakati kwa VIP A itakuwa ni sh. 20,000.


Hiyo itakuwa ni mechi ya mwisho ya majaribio kwa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kabla ya kwenda jijini Harare kwa ajili ya mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika dhidi ya Zimbabwe (Mighty Warriors).


Malawi (Flames) inayonolewa na mchezaji wake wa zamani Young Chidmozi nayo itakuwa inacheza mechi ya mwisho ya majaribio kabla ya kwenda N’djamena kuikabili Chad.

No comments:

Post a Comment