STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

Sikinde kutambulisha mpya TZF Kigogo

Waimbaji wa Sikinde, Abdallah Hemba, Hassan Bitchuka
Bitrchuka (kushoto) akiimba huku Adolph Mbinga akicharaza gitaa
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Wana Sikinde' keshokutwa inatarajiwa kutambulisha nyimbo mpya kwa mashabiki wa  Kigogo ikiwa ni kwa mara ya kwanza ndani ya mwaka huu.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo aliliambia gazeti hili kuwa, Sikinde itatambulisha nyimbo hizo zitakazokuwa katika albamu yao ijayo na zile za  zamani.
Milambo alisema mashabiki wa muziki wa dansi wamekuwa wakituma maombi ya kupelekewa burudani na wao wameitikia na watafanya hivyo Jumatano.
"Sikinde inatarajiwa kufanya onyesho maalum la kutambulisha nyimbo mpya za albamu yetu ijayo pamoja na kukumbushia vibao vya zamani kwa mashabiki wetu wa Kigogo walioililia bendi yao kwa muda mrefu," alisema.
Milambo alitaja nyimbo zitakazotambulishwa kuwa ni 'Jinamizi la Talaka', 'Kibogoyo', 'Tabasamu Tamu', 'Deni Nitalipa', 'Za Mkwezi' na Nundule' ambazo zinamaliziwa kurekodiwa albamu mpya ya bendi hiyo iliyotoa albamu ya mwisho mwaka 2011.
Nyimbo za zamani zitakazopigwa katika onyesho hilo kwa mujibu wa Milambo ni 'Kassim', 'Selina', 'Salam kwa Wazazi', 'Mv Mapenzi', 'Supu Imetiwa Nazi', 'Maisha Mapambano', 'Edita', 'Naomi' na 'Clara'.
"Yaani itakuwa bandika bandua kwa nia ya kusuuza nyoyo za mashabiki wetu ambao walitukosa kwa muda mrefu," alisema.

No comments:

Post a Comment