STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 27, 2014

Masai ya Wapi anayejitoa kundini?!

Masai katika pozi
Masai Nyota Mbof

WAKATI akiwa mbioni kuachia video ya wimbo wake mpya uitwao 'Masai ya Wapi' alioimba na Christian Bella, mchekeshaji maarufu nchini, Gilliad Severine 'Masai Nyota Mbofu' ametangaza kujiengua Al Riyami Production.
Akizungumza na MICHARAZO, Masai anayetamba na nyimbo za 'Rungu na Mukuki' na 'Yero Masai' aliouachia hivi karibuni, alisema ameamua kujiengua Al Riyami inayoendesha vichekesho vya 'Vituko Show' kutokana na kutoridhishwa na hali ya mambo na sasa atajitegemea hadi atakapotua kundi au kampuni nyingine ya uigizaji.
Masai alisema kuondoka kwake hakuna maana kama kuna ugomvi na yeyote ila ameamua kubadilisha upepo na kujikita zaidi kwenye  muziki, japo ataendelea kucheza filamu kwa yeyote atakayemhitaji.
Kuondoka kwa Masai kumezidi kulidhoofisha kundi hilo kwani kabla ya hapo wakali kama akina KItale, Mzee Majuto, Kingwendu, Ringo na Gondo Msambaa nao walijeingua kwa nyakati tofauti, huku wasanii wengine wakipunguzwa kundini humo kwa sababu mbalimbali.
Kuhusu kazi yake mpya, Masai alisema kwa sasa anajiandaa kuitoa hadharani video ya wimbo wa 'Masai ya Wapi'.
Alisema amepanga kutoa video tu wa wimbo huo bila 'audio' yake kwa sababu zake na kwamba kazi hiyo mpya ameimba kwa kushirikiana na Christian Bella.
"Wakati video ya wimbo wangu wa 'Yero Masai' ikianza kubamba katika runinga, nipo katika maandalizi ya mwisho ya kukamilisha na kuiachia video nyingine ya wimbo wa 'Masai ya Wapi', huu sitatoa 'audio' yake," alisema Masai.

No comments:

Post a Comment