
WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya CECAFA Nile Basin Cup,Mbeya
City chini ya kocha mkuu Juma Mwambusi wamefungwa mabao 2-1 na AFC
Leopard ya Kenya katika mchezo uliopigwa usiku wa jana mjini Khartoum.
Bao la Mbeya City lilifungwa na kiungo mshambuliaji,Deus Kaseke, huku washindi wakitangulia kufunga mabao yao .
Ushindi huo unawafanya AFC Leopard wajikite kileleni mwa kundi B baada ya kufikisha pointi 6.
No comments:
Post a Comment