STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 14, 2014

'Bethidei' mtoto wa Kajala ya kipekee

MUIGIZAJI nyota nchini Kajala Masanja anatarajiwa kumsindikiza mtoto wake Paula kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kula bata na watoto wenye ulemavu wa akili wanaolelewa katika eneo la Sinza.
Kwa mujibu wa muongozaji na 'meneja' wa Kajala katika uzalishaji filamu, Leah Richard 'Lamata' Paula atasherehekea siklu yake ya kuzaliwa keshokutwa na Kajala ameamua kuiandalia sherehe hiyo kuwafariji watoto hao walemavu.
"Mtoto wa Kajala anatarajiwa kufanyiwa sherehe ya kuzaliwa kwake na mama yake yaani Kajala na shughuli nzima itafanyika katiia kituo cha kulelea watoto wenye Ulemavu wa akili Sinza, mtoto huyo atatumia siku hiyo kula na kucheza na watoto hao," alisema Lamata.
Lamata alisema Kajala ameamua kufanya hivyo kama njia ya kuwafariji watoto hao sambamba na kumpa darasa mwanae juu ya kutambua umuhimu wa kuwaheshimu na kuwajali watu wenye hali tofauti za kimaumbile na sherehe hiyo itahudhuriwa na watu mbalimbali wakiwamo nyota wa filamu nchini.

No comments:

Post a Comment