STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 14, 2014

NI UJERUMANI 2014, WANAUME WAWEKA REKODI BRAZIL

Ujerumani wakishangilia taji lao baada ya kuilaza Argentina na kutwaa Kombe la Dunia 2014

Raha Tupu kwa Wanaumeeeeee!
Vita ilikuwa naona hii pichani




UJERUMANI imeweka rekodi ya kutwaa taji la Kombe la Dunia katika Bara la Amerika ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu za Ulaya baada ya kuinyuka katika muda wa nyongeza Argentina waliokuwa waliopoiteza nafasi nyingi kuweza kumaliza kazi na kulibakisha taji hilo baranai humo.
Bao la dakika ya 113 kupitia kwa mtokea benchi  Mario Gotze lilitiosha kuwapa Ujerumani taji la nne la michuano hiyo huku wakiweka rekodi nyingine ya kucheza mechi zao saba bila kupoteza hata mchezo mmoja na ikiongoza kwa idadi kubwa ya mabao ya kufunga 18 na kufungwa manne tu.
Pambano hilo lililokuwa na kosakosa nyingi, Argentina ikipoteza nafasi nyingi za kufunga, lilishuhudia dakika 90 zikimalizika kwa sare ya 0-0 na kuongezwa dakika 30 za nyongeza.
Katika dakika hizo pambano liliwaweka roho juu mashabiki wa timu zote na Messi alikaribia kufunga bao la kusawazisha na pengine kuupelekea mchezo huo kwenye matuta, lakini Mchezaji Bora huyo wa michuano hiyo ya Brazili alipaisha kimaajabu mbele a Kipa Bora wa mashindano hayo ya 2014, Manuel Nieuer.
Mario Gotze aliyeingia uwanjani badala ya Miloslav Klose dakika mbili kabla ya muda wa kawaida kumalizika alipata pande safi ya Andre Schuerrle na kutuliza gambani kabla ya kumtungua kipa wa Argentina, Sergio Romelo.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ujerumani kunyakua taji hilo kama nchi kamili ya Muungano wa Ujerumani Mbili ambazo zilikuwa zimetengena kwani mataji yake matatu ya awali ya mwaka 1954, 1974 na 1990 ilinyakua kama Ujerumani Magharibi 
 

No comments:

Post a Comment