STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 14, 2014

Messi apozwa Brazil, 'James Bond' anyakua kiatu cha Dhahabu

James Rodriguez wa Colombia aliyetwaa kiatu cha dhahabu

Lionel Messi wa Argentina aliyeteuliwa kuwa MCHEZAJI BORA
NYOTA wa Argentina, Lionel Messi ambaye ameshindwa kutimiza ndoto za kunyakua Kombe la Dunia baada ya kunyakua kila aina ya tuzo katika maisha yake ya soka, amepozwa kwa kutangazwa kuwa MCHEZAJI BORA wa michuano ya Kombe la Dunia 2014. Messi aliyermaliza michuano hiyo akiwa na mabao manne sawa na Robin van Persie wa Uholanzi alinyakua tuzo hiyo akishuhudia timu yake ikishindwa kuizuia Ujerumani kunyakua taji la nne la michuano hiyo ikiwa kwenye ardhi ya Bara la Amerika ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu kutoka barani Ulaya. Naye James Rodriguez 'James Bond' licha ya timu yake kutolewa hatua ya Roboi Fainali na Brazili amefanikiwa kunyakua kiatu cha Dhahabu kutokana na kuwa MFUNGAJI BORA wa michuano hiyo akiwa ametupia mabao sita akimzidi Thomas Muiller wa Ujerumani aliyemaliza wa pili na mabao matano. Kipa shujaa wa Ujerumani, Manuel Nieuer licha ya kuisaidia timu ya Ujerumani kutwaa taji katika mchezo wa fainali dhidi ya Argentina, pia alinyakua tuzo ya KIPA BORA katika michuano hiyo ambayo itakumbukwa kwa msisimko mkubwa iliyokuwa nayo.
Naye winga matata wa Ufaransa, Paul Pogba alinyakua tuzo ya Mwanasoka Bora Chipukizi. Mkali huyo anakipiga Juventus na amaekuwa akihusishwa na mipango ya kutaka kujiunga na Chelsea.


No comments:

Post a Comment