STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 15, 2014

MAYWEATHER KURUDIANA NA MAIDANA SEPTEMBA.

BINGWA wa masumbwi wa uzito wa welter ambaye hajapigwa mpaka sasa, Floyd Mayweather anatarajiwa kucheza pambano la marudiano na Marcos Maidana wa Argentina. 
Mayweather mwenye umri wa miaka 37 raia wa Marekani anatarajiwa kutetea mikanda yake ya ubingwa inayotambuliwa na Baraza la Ngumi Duniani-WBC na Chama cha Ngumi Duniani-WBA dhidi ya maidana aliyemdunda katika pambano lililofanyika Mei 3 mwaka huu. 
Wawili hao wanatarajiwa kupambana tena jijini Las Vegas, Septemba mwaka huu. 
Akihojiwa Mayweather ametamba kuwa ana uhakika wa kushinda pambano hilo pamoja na kukiri kuwa utakuwa mpambano na mgumu. 
Katika pambano lililofanyika Mei, jaji wa kwanza alitoa alama 114-114, wakati majaji wawili waliobakia walitoa alama 116-112 na 117-111 ambapo alama zote za juu zilikwenda kwa Mayweather. 
Mayweather anakaribia kufikisha rekodi ya kucheza mapambano 49 bila kupigwa iliyowekwa na bingwa wa zamani wa uzito wa juu Rocky Marciano, ambapo mpaka sasa ameshashinda mapambano 46 bila kupigwa.

No comments:

Post a Comment