STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, July 15, 2014

'Shujaa' waa Ujerumani haamini kama wametwaa ndoo

KIkosi cha Ujerumani na kocha wao wakishangilia ubingwa
Mario Gotze akiwa na famnilia yake akishangilia ubingwa
 MUUAJI aliyeizamisha Argentina na kuipata timu yake ya Ujerumani ubingwa wa Kombe la Dunia Mario Gotze amesema ilikuwa ni ndoto iliyokua kweli baada ya kuisaidia Ujerumani kutwaa Kombe la Dunia kwa kufunga goli pekee la mechi ya fainali dhidi ya Argentina kwenye Uwanja wa Maracana juzi.
Kiungo huyo wa Bayern Munich alianzia benchi katika mechi hiyo hiyo, lakini aliingizwa mwishoni mwa kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Miroslav Klose.
Gotze hakumuangusha kocha Joachim Low na akafunga goli katika dakika ya 113 kufuatia krosi ya Andre Schurrle na kuwapa Ujerumani ubingwa wa nne wa Kombe la Dunia.
"Ni hisia za aina yake, sijui nizielezee vipi. Nilipiga shuti tu na sikujua nini kitatokea. Ni ngumu kuamini," alisema nyota huyo mwenye umri wa miaka 21.
"Kwetu sisi,ndoto imekua kweli. Najivunia timu na nina furaha ya kupindukia kwa kila kilichotokea Brazil.
"Kila mchezaji katika timu yetu anastahili kutajwa hapa na tunajivunia kutwaa kombe hili."
Gotze amecheza mechi sita za Kombe la Dunia 2014 na amefunga magoli mawili.

No comments:

Post a Comment