STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 17, 2014

Arsenal yaanza vyema England, Spurs yatusua ugenini




ARSENAL imeianza vyema Ligi Kuu ya England baada ya kuitandika Crystal Palace ilitimtimua kocha wake, Tony Pulis kwa mabao 2-1.
Mchezo huo ambao ulikuwa wa mwisho kwa pazia la ufunguzi la ligi hiyo usiku wa jana ilishuhudiwa wageni wakitangulia kupata bao kupitia Hangeland dakika 35, kabla ya Koscienly kusawazisha dakika 45. Kipindi cha pili Arsenal walitengeneza nafasi nyingi lakini wakashindwa kuzitumia vizuri na mpaka dakika 90 bado ilikuwa 1-1, dakika 5 za nyongeza Aaron Ramsey akaifungia Gunners goli la ushindi.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Tottenham Hotspur ikiwa ugenini imepata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya West Ham licha ya kiucheza pungufu kwa muda mrefu baada ya beki wake mmoja kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 29.
Bao pekee liliwekwa kimiani na Eric Dier katika dakika za ziada katika mechi iliyopigwa kwenye uwanja wa Boleyn Ground.

Stoke City ikiwa nyumbani kwake nayo ilijikuta ikilala kwa Aston Villa kwa kufungwa 1-0, bao likiwekwa kimiani na Andreas Weimann dakika ya 50.
Leicester City ilikaribishwa tena kwenye Ligi Kuu kwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Everton, huku QPR ikilala nyumbani bao 1-0 dhidi ya Hull City, bao hilo likiwekwa kimiani na James Chester katika dakika ya 52.

No comments:

Post a Comment